1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelenskiy akosoa uamuzi wa kuilegezea Urusi vikwazo

13 Machi 2026

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy aliye ziarani nchini Ufaransa amesema uamuzi wa Marekani wa kulegeza vikwazo kwa mafuta ya Urusi hautoi msaada wa kumaliza vita na kupatikana kwa amani ya kudumu nchini mwake.

Ufaransa Paris 2026 | Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akimkaribisha Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akimkaribisha Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy katika Ikulu ya Elysee, mjini Paris. Picha: Michel Euler/AP Photo/picture alliance

Serikali ya Marekani ilitangaza mapema leo kuyaruhusu mataifa duniani kununua mafuta ya Urusi ambayo yamewekewa vikwazo na nchi za magharibi tangu kuzuka kwa vita vya Ukraine.

Akizungumza na waandishi habari mjini Paris akiwa pamoja na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, Zelenskiy amesema uamuzi huo utaipatia Moscow zaidi ya dola bilioni 10 inazoweza kuzitumia kwa vita.

Mtazamo wa  Zelenskiy umeungwa pia mkono na Rais Macron pamoja na viongozi wengine wa Ulaya ambao wamekosoa hatua hiyo ya Marekani iliyochochewa na kupanda kwa bei za mafuta kutokana na vita vya Mashariki ya Kati.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW