Zelenskiy: Ukraine ilizaliwa upya baada ya uvamizi wa Urusi
24 Agosti 2022![Ukraine | Wolodymyr Selenskyj](https://static.dw.com/image/62878245_800.webp)
Matangazo
Zelenskiy amesema vita vitamalizika tu sio wakati mapigano yatasitishwa bali wakati Ukraine itakapoibuka mshindi.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 44 amesisitiza msimamo mgumu wa Ukraineambao unapinga aina yoyote ya makubaliano ambayo yatairuhusu Moscow kudhibiti maeneo iliyoyakamata tangu kuanza kwa vita miezi sita iliyopita, yakiwemo maeneo ya kusini na mashariki mwa Ukraine.
Ameapa kuwa Ukraine italikomboa eneo liliokamatwa katika mkoa wa viwanda wa Donbas mashariki mwa nchi hiyo pamoja na rasi ya Crimea ambayo Urusi iliikwapua mwaka wa 2014.