1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky: Mazungumzo ya amani ya Ukraine yatakuwa mazuri

14 Februari 2026

Rais wa UkraineVolodymyr Zelenskiy ameelezea matumaini kuhusu mazungumzo ya kuvimaliza vita kati ya nchi yake na Urusi yatakayofanyika wiki ijayo huko Geneva, Uswisi.

Deutschland München 2026 | Volodymyr Zelenskyy spricht auf der Münchner Sicherheitskonferenz
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky Picha: Thomas Kienzle/AFP

Zelensky amesema ana matumaini makubwa kwamba mazugnumzo hayo yanayosimamiwa na Marekani yatakuwa na uzito na yenye umuhimu mkubwa.

Hata hivyo rais wa Ukraine ameonyesha wasiwasi kwamba ni nchi yake tu ndio mara zote inatakiwa ikubali kupunjika ili kufikia muafaka.

Zelensky amesema jambo hilo halimfurahishi na amesisitiza kwamba Ukraine haitakubali kuachia maeneo yake ya mashariki.

Rais wa Ukraine ameyasema hayo katika hotuba yake kwenye Mkutano wa Usalama wa Munich.

Amesema Marekani ambayo inasimamia mazungumzo hayo ya pande tatu mara nyingi mada hiyo ya kufikia makubaliano hujadiliwa tu katika muktadha wa Ukraine na sio Urusi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW