1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky kawaita Wajerumani marafiki wa kweli

14 Mei 2023

Rais Volodymyr Zelenskiy wa Ukraine anasema Kyiv na washirika wake wa Magharibi wanaweza kuishinda Urusi kwenye vita mapema mwaka huu na ameishukuru Ujerumani kwa kuwa rafiki wakweli.

Deutschland | Wolodymyr Selenskyj erhält den Karlspreis
Picha: Piroschka van de Wouw/REUTERS

Zelenskiy aliyewasili mjini Berlin usiku wa kuamkia leo Jumapili amefanikiwa kupata msaada mkubwa wa kijeshi, ambapo serikali ya Ujerumani ilitangaza kitita cha euro bilioni 2.7 siku ya Jumamosi, ukiwa msaada mkubwa kabisa tangu Urusi kuanzisha uvamizi wake mwezi Februari 2022.Akizungumza kwenye mkutano wa pamoja na waandishi wa habari akiwa na mwenyeji wake Kansela Olaf Scholz wa Ujerumani, Zelenskiy amesema sasa ni wakati wa wao kuamua mwisho wa vita hivyo mwaka huu, na wananaweza kumfanya mvamizi kushindwa daima kwa mwaka huu.Kwa upande wake, Kansela Scholz alisisitiza ahadi ya Ujerumani kuendelea kuiunga mkono Ukraine kadiri itakavyohitajika, akipuuzia hali ya wasiwasi iliyokuwapo kabla kwenye mahusiano ya pande hizo mbili na kurukia suala jengine juu ya matarajio ya Kyiv kujiunga na Muungano wa Kijeshi wa NATO.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW