Zelensky kukutana na Meloni mjini Roma
15 Aprili 2026
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky atakutana na Waziri Mkuu wa Italia Georgia Meloni, siku moja baada ya kuizuru Ujerumani, ambapo yeye na Kansela Ujerumani Friedrich Merz walikubaliana kuimarisha ushirikiano wa ulinzi, hasa katika vita vya ndege zisizo na rubani.
Zelensky amesema kipaumbele kikuu cha kidiplomasia cha Ukraine ni kupata msaada wa washirika wake kununua na kujenga mifumo zaidi ya ulinzi wa anga.
Ameyasema hayo Jumatano alipofanya mikutano na viongozi wa Ulaya, huku Urusi ikiendelea na mashambulizi yake mabaya dhidi ya raia na miundombinu ya umma nchini Ukraine.
Zelenskyy alikuwa akitembelea miji mitatu mikuu ya Ulaya katika saa 48, akihakikisha ahadi za msaada zaidi wa kijeshi na kifedha kutoka Ujerumani na Norway kabla ya safari yake kwenda Italia.