1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky: Wanajeshi wa Urusi warejeshwa nyuma Sumy

13 Juni 2025

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema vikosi vyake vinawarejesha nyuma wanajeshi wa Urusi kwenye mkoa wa Sumy, ambao umeangukia mikononi mwa Moscow kwa wiki za hivi karibuni.

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine.
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine.Picha: Annegret Hilse/REUTERS

Kwenye ujumbe wake kwa njia ya video usiku wa kuamkia leo, Zelensky aliwashukuru wanajeshi kwa kile alichokiita mafanikio yao.

Vikosi vya Urusi vimekuwa vikisonga mbele ndani ya mkoa huo tangu mwezi Aprili, huku Rais Vladimir Putin akitaka lianzishwe eneo lisilo shughuli za kijeshi baada ya wanajeshi wa Ukraine kuondolewa kwenye mkoa wa magharibi mwa Urusi wa Kursk.

Soma zaidi: Pistorius akataa Ujerumani kubadili sera kuelekea Urusi

Pande zote mbili zimethibitisha kuwa Urusi imetwaa vijiji kadhaa vya mkoa wa Sumy, ambao umekuwa ukishambuliwa mara kwa mara na jeshi la anga la Urusi. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW