1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky yuko ziarani nchini Ufaransa

13 Machi 2026

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amewasili nchini Ufaransa leo asubuhi kwa mazungumzo na Rais Emmanuel Macron.

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine.Picha: ALESSANDRO DELLA VALLE/AFP/Getty Images

Mazungumzo hayo yatatuama juu ya kuongeza mbinyo dhidi ya Urusi ili kuilazimisha isitishe vita vilivyoingia mwaka wake wa tano.

Ziara yake inafanyika katika wakati mazungumzo kati ya Ukraine na Urusi yanayosimamiwa na Marekani yamekwama kutokana na vita vilivyozuka baada ya Marekani na Israel kuishambulia Iran.

Kulingana na Ikulu ya Ufaransa, Elysee, viongozi hao wawili watajadili uwezekano wa kuongeza vikwazo vya kiuchumi kwa Urusi hususani kwa kuzilenga meli zake zinazosafirisha mafuta kwa siri.

Mapema wiki hii Ikulu ya Urusi, Kremlin, ilikosoa mpango wa Zelenskykuitembelea Ufaransa ikisema ziara hiyo itatatiza mchakato wa amani unaoendelea na kuzitaja juhudi za kuongeza shinikizo kwa Moscow kuwa "jambo la kipuuzi." 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW