1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Zelenskyy asema hayapokea majibu ombi la mkutano na Putin

13 Mei 2025

Rais Volodymyr Zelenskiy wa Ukraine amesema bado hajapokea majibu kutoka Urusi juu ya ombi lake la kutaka akutane ana kwa ana na Rais Vladimir Putin nchini Uturuki baadaye wiki hii

Rais Volodymyr Zelenskiy wa Ukraine
Rais Volodymyr Zelenskiy wa Ukraine.Picha: Genya Savilov/AFP

Zelensky ameyasema hayo kupitia hotuba yake kwa taifa aloitoa usiku wa kuamkia leo. Ofisi yake imesisitiza Zelenskyy anataka kukutana na Rais Putin na siyo wawakilishi wengine wa Urusi, kwenye mazungumzo yaliyopendekezwa na Putin mwenyewe mwishoni mwa wiki iliyopita.

Hadi sasa Moscow haijasema chochote kuhusu uwezekano wa Putin kukutana na Zelensky siku ya Alhmisi mjini Istanbul. Wakati hayo yakijiri maandalizi ya awali ya mkutano kati ya pande hizo mbili yameanza kwa mazungumzo ya maafisa wa ngazi ya juu.

Hapo jana Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Urusi Sergei Lavrov alizungumza na mwenzake wa Uturuki Hakan Fidan huku mwanadiplomasia mkuu wa Marekani Marco Rubio alifanya mashauriano na mawaziri wenzake wa nchi za Ulaya ikiwemo, Uingereza na Ufaransa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW