Kandanda
Bado siku 100 kabla ya kuanza michuano ya kombe la dunia
3 Machi 2026
Matangazo
Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA limesema tiketi milioni mbili zimeshauzwa katika awamu mbili za kwanza za mauzo na mahitaji bado ni makubwa mno kiasi kwamba tiketi ziliagizwa zaidi kupita kiwango cha mara 30.
Gharama ya tiketi yapaa
Makamu wa rais wa chama cha mashabiki wa soka nchini Ufaransa Mehdi Salem,amesema wanashuhudia ongezeko la gharama za tiketi kwa zaidi ya asilimia 200 tofauti na kiasi walichoambiwa na shirikisho la soka la Ufaransa na FIFA mnamo mwaka 2018.