Bunge la Uingereza lina mpango wa kumdadisi mmiliki wa mtandao wa kijamii wa Facebook Mark Zuckerberg kutokana na utumiaji mbaya wa data ambao uliwaathiri watumiaji milioni 50 wa mtandao huo. Kampuni moja ya Uingereza Cambridge Analytica inayodaiwa kuhusika na kampeni ya Rais wa Marekani Donald Trump katika uchaguzi wa Marekani mwaka 2016 imetajwa kuhusika pakubwa katika sakata hiyo.